Kila mtu ana upendeleo wake likija swala la usafiri, ila
ukweli ni kwamba kila mmoja hutumia miguu kama usafiri kutoka sehemu moja
kwenda nyingine, “every one is naturally a pedestrian”. Barabara sio kwa ajili
ya magari na pikipiki pekee bali hata waenda
kwa miguu. Takwimu zinaonyesha kua waenda kwa miguu ni miongoni mwa wahanga
wakubwa wa ajali za barabarani. Hivyo ni muhimu kwa kila mtu kuwa na elimu
stahiki ya namna yakutumia barabara wakati wakutembea. Yafuatayo ni mambo
ya kuzingatia unapotembea barabarani; 1.
Tabirika,
fuata sheria na taratibu za barabarani na tilia maanani alama, ishara na
michoro ya barabarani; 2.
Pita
kwenye njia za pembeni kama zipo; 3.
Tembea
upande wa kulia mwa barabara ili uweze kuyaona vizuri na kupishana na magari
yanayotoka unakoelekea na iwe pembeni sana iwezekanavyo 4.
Onekana
muda wote, vaa nguo zinazong’aa wakati wa mchana na zinazo akisi mwanga wakati
wa usiku au tumia tochi; 5.
Angalia
magari yanayo ingia na kutoka barabarani au yanayo taka kuegesha au kutoka
kwenye maegesho. 6.
Epuka
ulevi wa aina yoyote ukiwa unatembea barabarani, itakupunguzia uwezo wa kufanya
maamuzi; 7.
Kuwa
makini muda wote, vyombo vya kielektroniki visikuchanganye, kawaida vyombo
hivyo huchukua masikio na macho yako barabarani, mfano “earphones” au “headphones”. Madhara ya kuweka “earphones” au “headphones” masikioni uwapo
barabarani ·
Hutosikia mingurumo ya gari hali inayoweza
kukusababishia kupata ajali; ·
Huhamisha akili yako kwenye kile unachokisikiliza
zaidi hivyo unaweza kujisahau kufuata kanuni na tarabibu stahiki uwapo
barabarani; ·
Ukipata taarifa ya mshtuko huenda ikakuathiri. Hasa
kama ulikua unatumia simu. Kuvuka
barabara a)
Tafuta
sehemu salama ya kuvuka b)
Fuata
kanuni za kuvuka barabara- Sehemu
salama kuvuka barabara ·
Mahali
ambapo kuna afisa wa polisi au mtu yeyote mwenye mamlaka anaeongoza magari.
Kumbuka kuwa ishara na maelekezo ya askari yanapaswa kupewa kipaumbele. Na mara
zote vuka mbele yao; ·
Kwenye
eneo ambalo kuna kivuko cha waenda kwa miguu (alama ya punda milia); ·
Kwenye
taa za barabarani ambazo utafuata ishara za taa hizo; ·
Madaraja
ya waenda kwa miguu na njia za chini; ·
Sehemu
ambapo unaweza kuona pande zote na ambapo watumiaji wengine wa barabara wanaweza
kukuona vizuri. Sehemu
ambazo siyo salama kuvuka barabara ·
Sehemu
ambapo kuna kizuizi kinachokuzuia kuona barabara vizuri pande zote. Mfano eneo
ambalo gari au magari yameegeshwa kama vile kwenye kituo cha mabasi; ·
Usivuke
barabara kwenye makutano ya barabara au njia panda; ·
Usivuke
barabara kwenye kona; ·
Usivuke
mbele ya magari ya dharura. Iwapo utayaona au kuyasikia magari ya wagonjwa,
magari ya zima moto, ya polisi au magari mengine yeyote ya dharura yenye
vimulimuli na sauti za ving’ora, usivuke
barabara mpaka yapite; ·
Kamwe
usivuke barabara moja kwa moja nyuma au mbele ya basi. Usivuke barabara na
basi. Acha mpaka lipite ili uweze kuona pande zote za barabara vizuri; ·
Usipande
juu ya uzio. Katika sehemu zingine za barabara uzio umewekwa ili kuwazuia watembea
kwa miguu kuvuka barabara na kuwaongoza mahali salama pa kuvuka. Usipande juu
ya uzio, au kutembea katikati yake na barabara. Vuka kwenye nafasi iliyowekwa. Fuata kanuni za kuvuka barabara ·
Simama
kwenye ukingo wa barabara; ·
Angalia
magari barabarani, upande wa kulia, kushoto, kulia tena sehemu zote kuzunguka,
na sikiliza mgurumo wa gari; ·
Kama
kuna gari linakuja liache lipite; ·
Angalia
tena upande wa kulia, kushoto kulia tena; ·
Baada
ya kufanya maamuzi ya kuvuka usitabiri kwamba dereva anakuona, wakati mwingine
inawezekana asikuone, kwa hiyo umakini ni juu yako na wakati wa kuvuka
hakikisha macho yako na ya dereva yamekutana na ameonesha dalili za kukuruhusu
uvuke mfano, kupunguza mwendo au kusimama; ·
Kuvuka
kwenye taa za barabarani. Katika baadhi ya sehemu kuna ishara za taa za
barabarani zinazo ongoza magari wakati wa kusimama na watembea kwa miguu wakati
wa kuvuka. wakati ishara ya mtu aliyewima mwenye rangi nyekundu inapooneshwa
USIVUKE. Wakati taa zikibadilika kuonesha ishara ya mtu anayetembea mwenye
rangi ya kijani, angalia kuwa magari yamesimama na kisha vuka kwa uangalifu.
Baada ya muda ishara ya rangi nyekundu, au wakati mwingine ishara ya rangi ya
kijani inawaka gafla, na hii maana yake usianze kuvuka, kwasababu magari karibu
yataanza kwenda tena. Iwapo taa za barabarani hazina ishara maalumu kwa
watembea kwa miguu, angalia kwa umakini na usivuke hadi taa nyekundu
itakapowaka na magari kusimama. Pamoja na hayo angalia magari yanayopinda kona.
Kumbuka kuwa taa za barabarani zinaweza kuruhusu magari kutembea kwenye baadhi
ya njia wakati njia zingine zikiwa zimesimama.